LULU APELEKWA MAHAKAMANI - BIGTYME
Headlines News :
Home » » LULU APELEKWA MAHAKAMANI

LULU APELEKWA MAHAKAMANI

Written By Appleconnect on Apr 11, 2012 | 7:46 PM


Pichani: Elizabeth Michael ‘Lulu’ akiwa katika Mahakama ya Mwanzo Kinondoni, Dar es Salaam mwaka jana alipokuwa akituhumiwa kumshambulia kwa matusi ya nguoni, mlalamikaji Kilakhaba Aziz.
Richard Bukos na Issa Mnally
Msanii maarufu wa filamu hapa nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’ leo amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa shitaka la mauaji.  
Lulu alipandishwa kizimbani kwa usiri mkubwa akitokea Kituo cha Polisi cha Oysterbay alikokuwa akishikiliwa na kupandishwa kizimbani moja kwa moja bila kuwekwa mahabusu ya mahakama hiyo kama iwavyo kwa washitakiwa wengine wanaosubiri kusomewa kesi zao.
Baada ya kupandishwa kizambani alisomewa shitaka lake na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama hiyo, Elizabeth Kaganda ambapo alisema Mnamo Aprili 7 mwaka huu majira ya saa saba za usiku maeneo ya Sinza Vatican jijini Dar es Salaam Elizabeth Michael (18) alimuua Steven Kanumba. Katika kesi hiyo mshitakiwa hakutakiwa kujibu lolote isipokuwa alinyoosha kidole na kupinga umri uliotajwa kuwa ana miaka 18 na kusema umri wake ni miaka 17. Baada ya kusomewa shitaka hilo, Lulu alipelekwa gerezani Segerea na kesi yake itasikilizwa tena aprili 23 mwaka huu.
Share this article :

1 comment:

  1. Рerhaps thiѕ is partiаlly respοnsіble for thе еxpensiѵe unit, it's a TENS nuisance fill-in- a twist that's ԁesignеd to іntercept thе torso's painfulness signals received by the learning ability to change how it perceives the aesthesis. Last, many users relish the reposeful massage that it provides, and how does it act?
    My website > http://aurawavereview.com/

    ReplyDelete

'Thanks for visiting please leave a comment'

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. BIGTYME - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Sopsop Media